Katika miaka ya 1990 na 2000, nyimbo zao kama "Nuhu", "Hivi Vita Vimekoma”, "Ilikuwa Alfajiri", “Shangilieni” na "Habari ya Mwana Mpotevu" zilipata umaarufu mkubwa, hasa wakati wa sikukuu za Kikristo kama Krismasi na Pasaka. Nyimbo hizi ziliwasaidia waumini wengi kuelewa na kuhisi ujumbe wa injili kwa njia ya kipekee.
Baadhi ya wanakwaya wa Shangilieni kwaya Arusha.
Hadi leo, Tumaini Shangilieni Choir inaendelea kutoa albamu mpya na nyimbo kwenye majukwaa mbalimbali mtandaoni kama vile YouTube na majukwaa mengine. Albamu yao ya hivi karibuni, "Yupo Mungu", iliyotolewa mwaka 2023, ina nyimbo kama "Yesu Ee", "Ewe Moyo Wangu", na "Kama Si Wewe Bwana".
Mchango wa Tumaini Shangilieni Choir katika muziki wa injili nchini Tanzania ni wa thamani kubwa, na nyimbo zao zinaendelea kuwa baraka kwa vizazi mbalimbali mpaka leo hii.
0 Comments